Kwa Tanzania ni kosa la jinai kutupa au kutekeleza mtoto mchanga, na sio Tanzania pekeake, sehemu nyingi Duniani ukitelekeza au kutupa mtoto sio kesi ya kusamehewa hata kidogo !!
Jeaneta Bente ni mama wa watoto mapacha watatu, alijifungua na kuwatelekeza watoto wake wote Hospitali iliyoko Jiji la Drobeta Turnu-Severin, nchi ya Romania.

Mama huyo alijifungua mapacha hao Alexandra, Isabela na Cristina salama kabisa japo watoto wote walizaliwa njiti yani hawakutimia miezi tisa… aliamua kutoroka na kukimbia Hospitali huku akiwatelekeza watoto hao wachanga.
Baadae taarifa ya watoto kutelekezwa ikagusa kwenye stori za Vyombo vya Habari, mama akaamua kurudi na kuongea ukweli sababu iliyofanya awatelekeze watoto wake Hospitali >>>’Naamini watu watanielewa kwamba sina uwezo wa kuwatunza na kuwahudumia… Nawatakia kila la heri na ninaamini watakuwa na maisha mazuri zaidi ya vile ambayo mimi ningewalea‘ >>> hii ndio sentensi aliyonukuliwa Jeaneta Bente akijitetea kuhusu kuwatelekeza watoto wake.
Ripoti za Hospitali za Romania zinaonesha kumekuwa na ongezeko kubwa la watoto wanaotelekezwa na wazazi wao huku wakitoa sababu moja kubwa kwamba hawana uwezo wa kuwalea watoto wao… Uamuzi uliofatia ilikuwa ni kuwachukua watoto hao na kuwapeleka kwenye nyumba ambazo wanalelewa watoto wasio na wazazi na waliotelekezwa.
Hizi ni pichaz za mazingira ya mama huyo anapoishi.
PAPO KWA PAPO zipate habari zote zinazonifikia kuanzia kwenye siasa muziki, michezo, maisha, Breaking news na nyingine kwa kujiunga hapa na mimi >>> Twitter Insta FB na nitakua nikikutumia kila ninachokipata, pia usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>YouTUBE