Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sixtus Mapunda amefanya ziara fupi ya kutembelea maeneo yalioathiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini sambamba na kutoa wito kwa Wakazi wa Wilaya ya Temeke kuhama katika maeneo ya mabondeni kwani ni hatari kwa kipindi hiki cha mvua.
Hayo yamesemwa leo April 26 katika Kata ya Toangoma mtaa wa Goroka wakati wa ziara fupi Mkuu wa Wilaya ametoa pole kwa Ndugu na Wakazi wa Toangoma kufatia vifo vya watu 4 walioangukiwa na ukuta, Wanawake 3 na Mwanaume 1.
” Naomba nitoe pole kwa Wanafamilia na Wakazi wote wa Eneo la Toangoma kwa kuondokewa na Wapendwa wetu lakini pia nitoe wito kwa Wanaioshi maeneo ya mabondeni kuhama haraka kwani ni hatari zaidi kwa kipindi hichi ambacho mvua zinaendelea kunyesha nchini na hata nje ya nchini” Amesema DC Mapunda.
Hata hivyo naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Goroka B amewataka Wanafamilia na Wakazi wa Goroka kata ya Toangoma kuwa na moyo wa uvumilivu hasa katika kipindi hichi ambacho wameondokewa na ndugu zao lakini pia kuzidi kuchukua Tahadhari juu ya mvua ambazo zinaendelea kunyesha.
Naye mchungaji Mzee Kisimini ambaye amezungumza kwa niaba ya Wachungaji wa Makanisa Manne ambayo yameshiriki katika uokoaji Wameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke kwa kutoa salamu za rambirambi kwa Wafiwa kiasi cha Tsh. Million 1 sambamba na Majeneza ya kuhifadhia miili yao.