Nchini Senegal, watu milioni 7.3 wanatarajiwa kupiga kura Machi 24, 2024, kuamua kati ya wagombea 17 ambao bado wako kwenye kinyang’anyiro cha kumrithi Macky Sall, ambaye ameongoza nchi hiyo tangu mwaka 2012. Hapo awali uchaguzi huu wa urais uliopangwa Februari 25, uliahirishwa kufuatia mzozo mkubwa wa kisiasa.
Kuna wagombea 17 ambao wanaenelea kushiriki kinyang’anyiro hiki cha urais kumrithi Macky Sall: Amadou Ba, Boubacar Camara, Aliou Mamadou Dia, Mamadou Lamine Diallo, El Hadji Mamadou Diao, Mahammed Boun Abdallah Dionne, Déthié Fall, Papa Djibril Fall, Bassirou Diomaye Faye, El Hadji Malick Gakou, Serigne Mboup, Daouda Ndiaye, Aly Ngouille Ndiaye, Anta Babacar Ngom, Khalifa Sall, Thierno Alassane Sall, Idrissa Seck.
Vituo 16,440 vya kupigia kura vinatarajiwa kufunguliwa Machi 24, pamoja na 807 nje ya nchi. Matokeo ya muda ya duru hii ya kwanza yatatangazwa kabla ya Ijumaa Machi 29.
Katika tukio la duru ya pili, hii itaandaliwa Jumapili ya pili baada ya Baraza la Katiba kutangaza matokeo ya mwisho ya duru ya kwanza.