Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: VIDEO: Kauli ya Waziri wa Kilimo kuhusu hali ya chakula na ukame nchini
Share
Notification Show More
Latest News
Waziri Mkuu ashtukia mchezo mchafu Kigoma, ‘zinapotea kinyemela, naleta timu’
September 22, 2023
Waziri wa Michezo, Dkt Damas Ndumbaro ajiuzulu nafasi hii kwenye uongozi wa TFF
September 22, 2023
GSM Home wamekuletea ‘Gulio la Kibabe’, haijawahi tokea wahi sasa, Ommy Dimpoz afunguka
September 22, 2023
Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta
September 22, 2023
Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou
September 22, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Mix > VIDEO: Kauli ya Waziri wa Kilimo kuhusu hali ya chakula na ukame nchini
Mix

VIDEO: Kauli ya Waziri wa Kilimo kuhusu hali ya chakula na ukame nchini

January 16, 2017
Share
3 Min Read
SHARE

Baada ya kuwepo taarifa za njaa na ukame uliosababishwa na ukosefu wa mvua kwenye maeneo mengi nchini, leo January 16, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amelazimika kutoa ufafanuzi kuhusu hali ya chakula nchini huku akisisitiza kuwa Tanzania ina chakula cha kutosha na haina shida ya njaa.

Waziri Tizeba amesema kuwa watu wanaoeneza taarifa za kuwepo kwa njaa Tanzania wana lengo la kuingiza mahindi yao yasiyo na ubora ili wafanye biashara, jambo ambalo serikali imelikataa.

Akizungumzia uhalisia wa hali, amesema kilichotokea ni kupanda kwa bei ya mahindi, hali iliyosababishwa na uamuzi wa serikali kuuza nafaka hiyo katika mataifa jirani yaliyokuwa na uhitaji mkubwa, ingawa kiwango kilichouzwa kilikuwa ni sehemu ya mahindi ya ziada.

“Mwaka jana gunia la mahindi kwa bei ya wastani wa kitaifa ilikuwa 65,000 lakini sasa ni 85,000 na wala haijafikia mara mbili mara tatu kama inavyosemwa ingawa kuna maeneo kama rorya imefikia hadi 150,000 kutokana na wao kutegemea misimu miwili wakajikuta wanatumia akiba yao lakini hali ya hewa ikawa tofauti kwahiyo kuna wafanyabishara wakaamua kutumia hiyo fursa kupandisha bei zaidi”

“Mavuno ya nafaka yalikuwa tani milioni 16 wakati mahitaji yakiwa tani milioni 13 kwahiyo ziada ilikuwa tani milioni 3, kwahiyo katika hiyo ziada milioni 1.5 ikasafirishwa nje, wenzetu walikuwa wananunua kwa gharama yoyote kwa kuwa walikuwa na shida, hiyo ndiyo maana bei ya nafaka imepanda sana hasa mahindi, kwa sasa bei imefika hadi mia 8 mia 9 na wauzaji ni walewale, kwahiyo hawezi kuuza ndani kwa bei ya chini lakini kupanda huko kulitarajiwa” – Waziri Charles Tizeba

Kuhusu ukame, amesema ni kweli kuna hali ya upungufu wa mvua, na hiyo inafahamika maana ilishatabiriwa na kuwataka wananchi watunze akiba yao ya chakula na wasidanganyike kukiuza, kwa sababu hali ya hewa haitakuwa nzuri katika baadhi ya maeneo.

Amewasihi wananchi waache tamaduni ya kung’ang’ania chakula cha aina moja na kuwataka kutumia vyakula vingine kama mahindi yamepanda bei.. “Nafaka siyo mahindi tu, tunao mchele na mpunga wa kutosha, na viazi vipo kutoka Tunduma, watumie hivyo”

Waziri Tizeba huyo amepiga marufuku mtu yoyote kutoa taarifa za njaa kwa kuwa serikali ndiyo inayojua hali ya chakula kupitia vyanzo vyake.

Kufahamu kila kitu alichozungumza Waziri Tizeba, bonyeza play hapa chini kutazama.

VIDEO: Yapo hapa Magazeti yote ya leo, na David King ameyachambua yote. Unaweza kutazama hapa chini.

You Might Also Like

Mradi wa Umeme wa Upepo wa Zanzibar wapamba moto

Joe Biden atuma salamu za pole kwa Mfalme wa Morocco

Rais Samia azindua ujenzi wa soko la Kizimkazi

EWURA yaridhishwa na kazi ya utengenezaji matela ya kusafirishia mabomba ya EACOP

NIC washinda tuzo 7 ndani ya mwaka 2023

TAGGED: Njaa, siasa, Ukame, Wizara ya Kilimo
Admin January 16, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Air Tanzania imeanza kwenda Dodoma, fahamu 165000 na 299000 zitavyofanya kazi
Next Article MJ Records imetambulisha ‘Kundi’ Jipya Bongoflevani..
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Waziri Mkuu ashtukia mchezo mchafu Kigoma, ‘zinapotea kinyemela, naleta timu’
Top Stories September 22, 2023
Waziri wa Michezo, Dkt Damas Ndumbaro ajiuzulu nafasi hii kwenye uongozi wa TFF
Top Stories September 22, 2023
GSM Home wamekuletea ‘Gulio la Kibabe’, haijawahi tokea wahi sasa, Ommy Dimpoz afunguka
Top Stories September 22, 2023
Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta
Sports September 22, 2023

You Might also Like

Sports

Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou

September 22, 2023
Sports

Xavi kuongeza mkataba wa Barcelona hadi 2025

September 22, 2023
Top Stories

Kuelekea fainali ya polisi jamii DPA cup mashabiki wajigamba afisa michezo atoa neno

September 22, 2023
Top Stories

UN yaitaka Iran kuachana na sheria mpya kuhusu hijab

September 22, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?