Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: “Hali ya uchumi wa nchi ni mbaya mno…inadidimia” – Zitto Kabwe
Share
Notification Show More
Latest News
Basata wafika kwenye msiba wa H Mbizo Morogoro, ‘Mazishi ni Dar’
January 28, 2023
The After Party ya Marioo kufanyika Elements Bar Masaki DSM Usiku wa leo
January 28, 2023
Picha: Katibu Mkuu wa CCM amewasili Wilayani Gairo Mkoani Morogoro
January 28, 2023
Uamuzi wa Baraza la Mashekhe Mkoa kuhusu Ndoa ya Dr Mwaka na Queen Masanja
January 28, 2023
Ukatili wa Wanafunzi shuleni, “Maafisa Elimu wapewa rungu”, washughulikieni Walimu
January 28, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > “Hali ya uchumi wa nchi ni mbaya mno…inadidimia” – Zitto Kabwe
Top Stories

“Hali ya uchumi wa nchi ni mbaya mno…inadidimia” – Zitto Kabwe

October 10, 2017
Share
6 Min Read
SHARE

Baada ya Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kutoa taarifa ya hali ya kiuchumi wa nchi ilivyo hivi sasa, leo October 10, 2017 Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe kupitia account yake ya Facebook alitoa maoni na ushauri katika hilo.

Zitto alinukuliwa>>>”Uchumi wa Nchi Unazidi Kudidimia, Thamani ya Shilingi Yashuka, Mfumuko wa Bei Wapanda“

“Jana Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ilitoa taarifa yake juu ya hali ya uchumi wa nchi yetu, taarifa iliyolewa inaonyesha hali si nzuri, uchumi wa nchi yetu unaonyesha kusinyaa na kudidimia, mfumuko wa bei unaonyesha kupanda na thamani ya shilingi kudidimia.”

“Taarifa hiyo inaonyesha namna hali ya uchumi wetu inavyozidi kuwa mbaya zaidi kwa wananchi wa hali ya chini , kwa mfumuko wa bei umepanda mno tangu kuanza kwa utekelezaji wa bajeti ya 2017/18, ongezeko ambalo limechangiwa zaidi na kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula (bidhaa ambazo wananchi wengi zaidi wanazitumia).”

“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia ongezeko hilo ni dagaa asilimia 7.6, matunda makavu kama nazi kwa (3.1), viazi vitamu kwa (3.0), mchele (1.5) na ndizi (1.5). Bidhaa nyingine zilizochangia ni mkaa kwa asilimia 4.0, dizeli (2.4) na petroli (0.6). Ukizitazama bidhaa zote hizi ni zile ambazo zinatumiwa zaidi na wananchi wa kawaida kabisa. Hivyo gharama za maisha kwa wananchi wa kawaida zimepanda mno, ufukara kutopea na familia zitakazoweza kupata angalao milo miwili kwa siku kupungua zaidi.“

“Taarifa imeonyesha thamani ya sarafu ya Tanzania imeshuka, uwezo wa Tsh. 100 kununua bidhaa umeshuka hadi Tsh. 92.18. Maana yake ni kuwa mwaka 2016 shilingi 100,000 ilikupa bidhaa za shilingi 100,000. Mwaka huu 2017 shilingi 100,000 inakupa bidhaa za shilingi 92,000. Kwa hiyo ili upate bidhaa za shilingi laki moja inakubidi uongeze shilingi elfu 8 zaidi. Kiuchumi, ili kulinda hali za wananchi, mishahara ilipaswa kupanda kwa asilimia 8 ili kuwapunguzia maumivu ya gharama za maisha.“

“Lakini hali hiyo inatokea katika wakati ambao mishahara haijapanda, na Rais wa nchi yetu kasema Serikali anayoingoza haitapandisha kabisa mishahara. Hali ni mbaya mno mtaani, mijini uzalishaji wa bidhaa za viwanda umeshuka kwa zaidi ya nusu, kutoka trilioni 1.5 mpaka bilioni 700 tu.”

“Siku za karibuni tumeshuhudia makampuni yakipunguza wafanyakazi na mengine kufungwa. Pia Serikali yenyewe ilipunguza watumishi iliyowaita hewa na wenye vyeti feki. Hivyo hivi sasa kuna Watanzania wengi mtaani ambao hawana shughuli zinazowaingizia kipato, tayari Wawekezaji wakubwa nchini wameshaitaka Serikali kutazama upya utendaji wake ili kuweka mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji ambao unashuka mno.”

“Vijijini tunashuhudia ushukaji wa sekta ya Kilimo kuliko wakati wowote ule tangu baada ya Uhuru. Wakulima wa Korosho hawajapewa pembejeo, hivyo uzalishaji wa zao linalotuingia mapato ya Kigeni zaidi nchini utashuka msimu huu wa mavuno, Tumbaku (zao la pili Kwa kuingiza Fedha za kigeni) tayari wakulima wanalia, mazao ya choroko na kunde bei imeshuka kwa zaidi ya 500%, Pamba uzalishaji umeshuka Kwa 63% kati ya mwaka 2015 na 2017 (miaka miwili ya awamu ya tano), Karafuu nayo mauzo yameshuka zaidi, na mauzo Nje ya dhahabu kuanza kushuka na hivyo kupelekea shilingi kushuka thamani na hivyo mfumuko wa bei kupanda Kwa kasi.“

Nini Kifanyike?

“1. Serikali itazame namna inatekeleza mipango yake ya Maendeleo. Uwekezaji kwenye miradi mikubwa ni jambo jema sana nchini kwani miradi mikubwa huingiza fedha kwenye mzunguko na hivyo kuchochea uchumi. Hata hivyo maarifa yanatakiwa kwenye miradi hii. Hapa nchini kwetu miradi mikubwa inaondoa Fedha kwenye uchumi na kupeleka Nje ya Nchi, tena Kwa Fedha za kigeni. Mfano Reli na Ndege ni miradi inayoondoa Fedha Nchini kwa dola na sio kwa madafu. Badala ya miradi hii kuwa ahueni inakuwa hasara kwa Nchi yetu.”

2. “Serikali isikilize na kufanyia kazi mawazo ya sekta binafsi katika kuweka sawa mazingira ya Uwekezaji bila kupoka haki ya Nchi kufaidika na rasilimali zake. Kwa mfano hoja aliyotoa Ndugu Dangote sio ya kupuuza kwani kwa kawaida Mitaji huona aibu (capital is shy). Serikali ijiondoe kwenye mentality kuwa Uwekezaji ni kupata kodi tu, la hasha. Kwa demografia ya Tanzania, ambapo watu milioni 1.6 huingia kwenye soko la ajira kwa mwaka, Ajira yapaswa kuwa lengo kubwa la Serikali katika kuvutia mitaji kutoka nje na vile vile ndani.”

“3. 3 Serikali ifanyie kazi haswa uchumi wa vijijini kwa kurekebisha mapungufu yote yanayoshusha uzalishaji kwenye sekta ya kilimo, kuanzia pembejeo, masoko na viwanda vidogo vya kuongeza thamani ya mazao (agro processing industries).”

Kwa Watanzania wenzangu,

“Kama Kiongozi wa watu hali hii ya kudidimia kwa uchumi wetu inaniumiza sana, nayaelewa maumivu mnayoyapata wananchi, wajibu wangu ni kupaza sauti ili Serikali ichukue hatua kupunguza makali haya ya hali mbaya ya uchumi. Mimi na chama ninachokiongoza, ACT Wazalendo, hatutaacha wajibu huo wa kuyasemea masuala yenu wananchi, hiyo ni ahadi yetu kwenu wananchi, tutaendelea kuwasemea.“

DIWANI MWINGINE KAWAJIBU LEMA NA NASSARI, KATOA SIKU SABA

You Might Also Like

Picha: Katibu Mkuu wa CCM amewasili Wilayani Gairo Mkoani Morogoro

Uamuzi wa Baraza la Mashekhe Mkoa kuhusu Ndoa ya Dr Mwaka na Queen Masanja

Ukatili wa Wanafunzi shuleni, “Maafisa Elimu wapewa rungu”, washughulikieni Walimu

Tazama Shaka alivyokula kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa “Sitotoa siri”

Mapya ndoa ya Dr Mwaka haijavunjwa, tamko kali latolewa na baraza la Ulamaa

TAGGED: Social media NEWS, TZA HABARI, Zitto Kabwe
Admin October 10, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Una mpango kujiunga Elimu ya Juu? Fahamu good news iliyotangazwa leo
Next Article Kama wewe ni Mwajiri kuna hii ya kufahamu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Basata wafika kwenye msiba wa H Mbizo Morogoro, ‘Mazishi ni Dar’
Entertainment January 28, 2023
The After Party ya Marioo kufanyika Elements Bar Masaki DSM Usiku wa leo
Entertainment January 28, 2023
Picha: Katibu Mkuu wa CCM amewasili Wilayani Gairo Mkoani Morogoro
Top Stories January 28, 2023
Uamuzi wa Baraza la Mashekhe Mkoa kuhusu Ndoa ya Dr Mwaka na Queen Masanja
Top Stories January 28, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Katibu Mkuu wa CCM amewasili Wilayani Gairo Mkoani Morogoro

January 28, 2023
Top Stories

Ukatili wa Wanafunzi shuleni, “Maafisa Elimu wapewa rungu”, washughulikieni Walimu

January 28, 2023
Top Stories

Tazama Shaka alivyokula kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa “Sitotoa siri”

January 27, 2023
Top Stories

Mapya ndoa ya Dr Mwaka haijavunjwa, tamko kali latolewa na baraza la Ulamaa

January 27, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?