Mengine kutoka Afrika Kusini pamoja na picha 12 hali ilivyokua
Share
2 Min Read
SHARE
Mitandaoni kumekuwa na picha na video nyingi zimesambaa zikionesha hali ilivyokuwa Afrika Kusini kwa zaidi ya wiki moja, tumesikia na kuona mashambulizi ambayo wamefanyiwa watu ambao sio raia wa Afrika Kusini ndani ya nchi hiyo, video nyingi na picha zinasikitisha.. watoto wanauawa, wanajeruhiwa.. vurugu ilikuwa kubwa sana.
Hapa ni ndani ya Kambi ya muda ambayo wamehifadhiwa wageni, yani walikuwa na maisha yao kawaida tu mtaani baadae wanajikuta ni wakimbizi.
Cha mwisho kilichonifikia ni kuhusu ishu ya Waziri wa Usalama wa South Africa, Nosiviwe Mpisa-Nqkula kutangaza kwamba sasa wanaoingia kupambana na watu wanaofanya vurugu hizo ni wanajeshi baada ya kuonekana kama Polisi wameelemewa nguvu na hali ilivyo mitaani, watu saba waliripotiwa kufariki pia.
Baadhi ya watu waliokusanyika kulaani mashambulizi ya wageni ndani ya Afrika Kusini.Mtaani hali haikuwa sawa, hili ni sehemu ya kundi kubwa la watu waliokuwa wanaandamana kupinga Xenophobia, ubaguzi wa kutaka wageni waondoke Afrika Kusini.Akina mama na watoto wao, wako kwenye foleni kusubiri chakula cha msaada ndani ya Kambi ya wakimbizi ambayo wamehifadhiwa kwa muda.Waandamanaji wakiwa na silaha, hali haikuwa shwari hata kidogo kwa wageni.Askari wakiendelea na zoezi la kuwakamata watu wanaochochea mashambulizi ya wageniMmoja ya majeruhi akipatiwa huduma ya dharura ya matibabu.Hali ilivyo kwenye Kambi walizohifadhiwa wageniFoleni ya kupokea chakula cha msaada ndani ya KambiWaandamanaji na silaha zao mtaani
Mfalme wa Wazulu, Goodwill Zwelithini. Analaumiwa kusababisha machafuko yaliyotokea Afrika Kusini kutokana na kauli yake aliyoisema kwamba wageni wanatakiwa warudi kwao. Jumatatu April 22 amekanusha kushinikiza machafuko hayo
Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membealisema kuna Watanzania waliouawa lakini mauaji hayo hayakutokana na vurugu hizi za kuwakataa wageni.
Pole kwa watu wetu wote ambao wameathirika kutokana na vurugu hizi.