Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: KESI YA BIL.1 :Maimu wa NIDA na wenzake waachiwa huru,wakamatwa tena(+video)
Share
Notification Show More
Latest News
Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama
February 2, 2023
Habari kubwa Magazetini Kenya leo February 2, 2023
February 2, 2023
Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha
February 2, 2023
Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro
February 2, 2023
Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu
February 2, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > AyoTV > KESI YA BIL.1 :Maimu wa NIDA na wenzake waachiwa huru,wakamatwa tena(+video)
AyoTVStori KubwaTop Stories

KESI YA BIL.1 :Maimu wa NIDA na wenzake waachiwa huru,wakamatwa tena(+video)

January 28, 2019
Share
3 Min Read
SHARE

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA), Dickson Maimu na wenzake 6 kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi yao.

Washtakiwa hao wameachiwa chini ya kifungu cha 91(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mara baada ya kuachiwa vigogo hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na kusababisha hasara ya Sh.Bilioni 1.16 wamekamatwa tena.

Maombi ya DPP kuwaondolea mashtaka vigogo hao yamewasilishwa na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon mbele ya Hakimu Mkazi Janeth Mtega.

Wakili Wankyo amedai kuwa DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa hao, hivyo anawaondolea chini ya kifungu hicho.

Baada ya kuwaondolea mashtaka, Hakimu Mtega alikubali ombi hilo ambapo washtakiwa wakaachiwa lakini wakakamatwa tena na kupelekwa mahabusu.

Kesi hiyo ilifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani Agosti18, 2017 lakini hadi sasa upelelezi.

Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo mbali na Maimu ni Meneja Biashara wa (NIDA), Avelin Momburi na Mkurugenzi wa TEHEMA, Joseph Makani.

Kwa pamoja washtakiwa walikuwa nane, lakini walibaki saba kwa sababu mmoja ambaye alikuwa Kaimu Mhasibu Mkuu wa NIDA, Benjamin Mwakatumbula alifariki dunia.

Wengine ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers, Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond na Xavery Kayombo.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kutumia madaraka vibaya, kula njama, kutumia nyaraka za uongo kumdanganya mwajiri na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh 1,169,352,931.

Inadaiwa kwenye shtaka la kwanza Maimu na Mwakatumbula kati ya Januari 15 hadi 19, mwaka 2010 katika makao makuu ya NIDA wilayani Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kwa nafasi walizokuwa nazo walitumia madaraka vibaya.

Wanadaiwa kuwa waliidhinisha malipo kwa Gotham International Limited (GIL) ya Dola za Marekani 2,700,00 bila ya kutumia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni vilivyowekwa na Benki Kuu ya Tanzania, kinyume na kifungu 19.3 cha mkataba kati ya NIDA na GIL, hivyo kuifanya GIL kupata faida ya Sh 3,969,000.

ILIVYOKUWA KESI YA WATOROSHA DHAHABU NA ASKARI WALIOTAKA RUSHWA BILIONI 1

You Might Also Like

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama

Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha

Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro

Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu

liganga na Mchuchuma ngoma nzito, Waziri akubali hoja za Askofu Gwajima

TAGGED: Ayo TV, Stori kubwa, Top Storie
Mika Ndaba TZA January 28, 2019
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Polisi wanadaiwa Milioni 51, Magereza MIL. 170, Mkurugenzi aiangukia Serikali (+video)
Next Article Yemi Alade akutana na Davido kwenye rekodi hii ya YouTube
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama
Top Stories February 2, 2023
Habari kubwa Magazetini Kenya leo February 2, 2023
Magazeti February 2, 2023
Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha
Top Stories February 2, 2023
Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro
Top Stories February 2, 2023

You Might also Like

Top Stories

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama

February 2, 2023
Top Stories

Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha

February 2, 2023
Top Stories

Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu

February 2, 2023
Top Stories

liganga na Mchuchuma ngoma nzito, Waziri akubali hoja za Askofu Gwajima

February 2, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?