October 12, 2016 Kenya inaingia kwenye headlines tena ikiwa ni baada ya mwimbaji staa wa Marekani Chris Brown kufanya show weekend iliyopita Mombasa, mpya ya leo imetoka kwa Gavana wa Mombasa Hassan Joho ambaye inaelezwa ndiye alidhamini tamasha la Mombasa Rocks Music Festival.

World TB day 2014
Gavana wa Mombasa, Joho Mohamed

Story kutoka 254 Kenya zinasema Gavana huyu inayedaiwa ana pesa za kutosha, ametangaza kuwa timu yake imeanza mazungumzo na uongozi wa rapper Nicki Minaj ili aje Mombasa kutumbuiza hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Nairobi Wire, Jamal Gaddafi aliyekua MC kwenye tamasha la Mombasa Rocks  Music Festival amesema amepewa taarifa na Joho, awambie mashabiki wajiandae kwa show nyingine kubwa ya Nicki Minaj.

http://media1.santabanta.com/full1/Global%20Celebrities(F)/Nicki%20Minaj/nicki-minaj-1a.jpg

Ripoti kutoka Kenya zinasema sababu kubwa hasa ya Gavana huyo kuwaleta mastaa wakubwa kutoka Marekani ni kutaka kukuza jina lake na kuitangaza zaidi Mombasa kwenye suala la utalii.

ULIPITWA NA MAJIBU YA MENEJA WA DIAMOND PLATINUMZ BAADA YA KUHUSISHWA KUZIMA MIC WAKATI ALIKIBA AKIIMBA? BONYEZA PLAY HAPA CHINI