Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Aweso afanya ukaguzi wa Barabara Tanga ‘Niliwahi kupiga hapa kuomba barabara, hatimae lengo limetimia’
Share
Notification Show More
Latest News
Aziz Ki Mfalme mpya town, mchezo dhidi ya Simba SC ya dhihirissha ubora wake, ‘Jemedari amwagia sifa’
August 14, 2022
Baada ya kipigo Ahmed Ally atoa kauli ya faraja kwa Wana Simba ‘Tunapitia maumivu makali mno’
August 14, 2022
Picha:Makamu wa Rais Philip Mpango ashiriki Marathon CRDB Bank 2022
August 14, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 14, 2022
August 14, 2022
Maneno ya Manara kuelekea Mchezo wa Yanga na Simba leo, “Nendeni mkapiganie Jezi na jina la Club’
August 13, 2022
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Waziri Aweso afanya ukaguzi wa Barabara Tanga ‘Niliwahi kupiga hapa kuomba barabara, hatimae lengo limetimia’
Top Stories

Waziri Aweso afanya ukaguzi wa Barabara Tanga ‘Niliwahi kupiga hapa kuomba barabara, hatimae lengo limetimia’

July 6, 2022
Share
6 Min Read
.
SHARE

MBUNGE wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso amemshukuru Rais Samia Suluhu huku akieleza kwamba utawala wake umekuwa ni suluhu ya matatizo ya watanzania na wana Pangani .

Aweso ambaye pia ni Waziri wa Maji aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kukagua na kutembelea ujenzi wa Barabara ya Tanga –Pangani-Bagamoyo kwa kiwango cha lami lenye kilomita 256.

Ambapo aliridhishwa na kasi ya utekelezaji wake inavyokwenda huku akiwahaidi ushirikiano wakandarasi wanaotekeleza mradi huo ili kuhakikisha ujenzi huo unakwenda kama ulivyopangwa.

.

“Wapo ambao walikuwa hawaamini kwamba ujenzi wa barabara hii utajengwa lakini leo hii hapa inajengwa na  Serikali inayoongozwa na  Rais Samia Suluhu tunamshukuru sana kwa hili kubwa alilotufanyia sisi wana Pangani”Alisema Mbunge Aweso.

Aidha aliwataka wana Pangani wachangamkie fursa za ujenzi wa mradi huo wa barabara kwa kuongeza uzalishaji zaidi kwa kutumia ardhi iliyopo kwa ajili ya kilimo  ikiwemo kuwataka kuacha kuuza maeneo yao kiholelaholela.

“Niwaombeni ndugu zangu sasa ujenzi huu unafanyika hii ni fursa na maendeleo kwa sababu itafungua fursa za kiuchumi hivyo niwasihi acheni kuuza ardhi kiholela holela kwa kuhakikisha mnayasimamia kutokana na fursa za kiuchumi zitafunguka wakati ujenzi huu utakapokamilika na kuweza kupata maendeleo”Alisema

.

Alisema kwa sababu ujenzi wa barabara hiyo unakwenda kuitoa Pangani pangoni na kuiinua kiuchumi na hivyo kufungua fursa za kimaendeleo hivyo wananchi hakikisheni mnaongeza uzalishaji.

“Niliwahi kupiga magoti hapa kuomba barabara hii lakini naishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Samia kwa kutufuta machozi wana Pangani kwa kuliona hili na utekelezaji wa mradi huu kwa sasa unaendelea na kubwa zaidi unakwenda pamoja- Waziri Aweso

.

“Nimeanza kukagua eneo la Choba nimeridhika sana na utekelezaji wake nifikisheni salamu za pongezi kwa Waziri wa Ujenzi Profesa Makame Mbarawa na Watendaji wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroad) kwa kuwapata wakandarasi wazuri wanafanya kazi vizuri”-Waziri Aweso

Aliongeza yeye kama mbunge wa Jimbo la Pangani aliwahaidi  wakandarasi hao kwamba watawapa ushirikiano kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati huku akiwaeleza kwamba changamoto ambazo aliwaeleza atakwenda kukutana na Waziri wa Ujenzi kuona namna ya kuzipatia suluhu.

Hata hivyo aliwapongeza Wakala wa Barabara nchini (Tanroad) mkoa wa Tanga kutokana na kwamba wanafanya kazi nzuri hasa juu ya usimamizi na ufuatiliaji wa mradi huu.

“Rais Samia ni Rais wa nchi nzima lakini ametambua kiu ya wananchi wa Pangani miaka ya nyuma ukitaka kwenda Pangani kutoka Tanga unacheza kiduku mpaka unafika Pangani kutokana na miundombinu mibovu ya barabara lakini ujenzi huo utaondosha changamoto hizo”- Waziri Aweso

.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroad) Mhandisi Zuhuru Amani alisema ujenzi wa barabara ya Tanga –Pangani kilomita 50 uligharimu kiasi cha Sh. bilioni 66.853 ambayo ilikuwa ni gharama za awali lakini imeongezeka na sasa kuwa Bilioni 67.458 kutokana na mabadiliko ya usanifu

Mradi huu ulipangwa kukamilika Novemba 14 mwaka 2021 lakini kutokana na sababu mbalimbali za kimkataba mufa wa kukamilika kwa mradi huo umeongezwa hadi Desemba 5,2022 na kazi hiyo inafadhiliwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100.

.

Alisema mradi huo mwanzoni ulikuwa ukisimamiwa na Mhandisi Mshauri M/S TECU (TANROADS Engineering Consulting Unit) hadi Desemba 5 mwaka 2020 na kwa sasa unasimamiwa na Mhandisi Mshauri M/S Dotch LTD ya Tanzania kwa gharama ya Sh.Bilioni 2.246 na utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimai 42.3 na hadi sasa mkandarasi amelipwa hati nne za madai zenye jumla ya Sh.Milioni 8.

Alisema awamu ya pili ya mradi huo ni ujenzi wa daraja la Mto Pangani  lenye urefu wa mita 525 utahusisha ujenzi wa barabara ya maungio ya daraja  yenye kilomita 14.3,barabara ya mchepuko ya kwenda ushongo kilomita 5.9 na barabara za Pangani mjini zenye urefu wa kilomita 5.4.

.
.
.
.
.

Mhandisi Zuhura alisema mradi huo unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Mkataba umesainiwa kati ya Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (Tanroad) na Mkandarasi M/s Shandong Luqiao Group Co.Ltd kutoka Chini Mei 5 mwaka huu kwa gharama zaidi Sh. Bilioni 82 kwa muda wa miezi 36 ya ujenzi na miezi 36 ya kipindi cha uangalizi kwa upande wa daraja ni miezi 12 kwa upande wa barabara.

Hata hivyo alisema kwa upande wa barabara ya Tungamaa –Mkwaja-Mkange kwa kiwango cha Lami (Km 95.2) ikijumuisha na barabara ya mchepuko ya Kipumbwi yenye kilomita 3.7 unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na mradi huo ulishasainiwa  na mtendaji mkuu wa wakala wa barabara nchini.

Alisema na mkandarasi M/s China Railway 15 Bureau Group Corporation  (CR15G) kutoka china kwa gharama za zaidi ya Sh.Bilioni 94 na kwa sasa muda wa miezi 36 ya ujnzi na miezi 12 ya kipindi cha uangalizi na kazi ya ujenzi imeanza Aprili Mosi mwaka huu na inatarajiwa kukamilika ifikapo Machi 31 2025 na zaidi ya Bilioni 14 zimelipwa kwa mkandarasi na mpaka sasa ikiwa ni malipo ya awali ya Mhandisi Mshauri kuidhinisha malipo hayo na utekelezaji wake umefikia asilimia 5.1.

You Might Also Like

Picha:Makamu wa Rais Philip Mpango ashiriki Marathon CRDB Bank 2022

Mauaji Moro: Mume amnyonga Mkewe na mtoto, Kaka wa Marehemu afunguka

Basi la New Force latumbukia korongoni, Mmoja afariki, Polisi anena chanzo

Ndugu abiria kulipwa Milioni 150, Wakili aibua mapya ‘Watu binafsi waliopost meme wajiandae’

Ajali Mbaya!! Watu sita wafariki, Polisi wafunguka, chanzo ‘Dereva alikuwa Mwendokasi, lilipinduka’

Edwin TZA July 6, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Mama asimulia ‘Chagulaga’ alivyotaka kumbaka rafiki yake, DC atoa maagizo mazito
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo July 7, 2022
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Aziz Ki Mfalme mpya town, mchezo dhidi ya Simba SC ya dhihirissha ubora wake, ‘Jemedari amwagia sifa’
Sports August 14, 2022
Baada ya kipigo Ahmed Ally atoa kauli ya faraja kwa Wana Simba ‘Tunapitia maumivu makali mno’
Sports August 14, 2022
Picha:Makamu wa Rais Philip Mpango ashiriki Marathon CRDB Bank 2022
Top Stories August 14, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 14, 2022
Magazeti August 14, 2022

You Might also Like

Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 12, 2022

August 12, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 11, 2022

August 11, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 10, 2022

August 10, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 9, 2022

August 9, 2022
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?