Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Utafurahi kuwaona Ronaldo na Messi wakicheza kikosi kimoja??
Share
Notification Show More
Latest News
Utacheka: Mwijaku apanda gari la Diamond ‘Rolls Royce’, Zuchu aangua kicheko, Baba Levo atia neno
August 19, 2022
Picha: Diamond ameingia makubaliano ya kudhamini mashindano ya Ndondo Cup
August 19, 2022
Kuelekea Sensa Agosti 23, Mbunge wa Jimbo la Ushtu anena hili kwa Wananchi wake
August 19, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 19, 2022
August 19, 2022
Kiwanda cha Chai Mponde Ujenzi wake umefikia 95%
August 18, 2022
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Sports > Utafurahi kuwaona Ronaldo na Messi wakicheza kikosi kimoja??
Sports

Utafurahi kuwaona Ronaldo na Messi wakicheza kikosi kimoja??

April 14, 2015
Share
3 Min Read
SHARE

ronaldo messi

Ulimwengu wa soka kwa miaka ya karibuni umetawaliwa na wachezaji wawili, mmoja wa FC Barcelona na mwingine ni mkali toka kikosi cha Real Madrid.

Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kwa pamoja wamekuwa katika kiwango ambacho kimewafanya waonekane kama watu wanaotoka kwenye sayari nyingine hali ambayo imezua upinzani kati yao.. story zao huwa hazikauki na kwenye HEADLINES za michezo, hata vijiweni pia.

Moja ya hoja ambazo zimekuwa zikiibuka ni nani kati ya wawili hawa ni bora kuliko mwingine, hoja hii imezaa swali jingine miongoni mwa watu ya kwamba ingekuaje kama wachezaji hawa wangekuwa kwenye timu moja??

Ni vigumu kwa hili kutokea kwani kwa sasa wanacheza kwenye timu zenye utamaduni wa upinzani na wanakoelekea ni vigumu kuona wakibadilishana timu siku moja yaani eti kumuona Ronaldo akichezea Barcelona na Messi akichezea Madrid ??

Sio hapo tu.. hata kwenye timu ya taifa uwezekano huo haupo kwani Messi ni Muargentina na Ronaldo anatoka Ureno.

mundo deportivo
Jarida la Mundo Deportivo limeripoti mpango wa kuandaa mchezo maalum wa wachezaji nyota barani ulaya .

Hata hivyo ndoto ya wawili hawa kuonekana wakichezea timu moja huenda ikawa kweli baada ya jarida moja la Hispania Mundo Deportivo kuripoti mpango wa kuandaa mchezo wa wachezaji nyota toka klabu mbalimbali barani ulaya.

Hii imetokana na wazo kama la mchezo wa Ligi ya Basketball Marekani NBA, yaani NBA All Star ambapo wachezaji huchaguliwa na kuwakilisha kambi za mashariki na magharibi na kwa Ulaya zitachaguliwa timu mbili zikiwakilisha wachezaji toka vilabu vya Ulaya Kaskazini na Kusini.

Wazo hili litahusisha wachezaji watakaochaguliwa na mashabiki kupitia mtandao ambapo kutakuwa na wastani wa wachezaji watatu toka klabu moja na hapa ndio uwezekano wa kuwaona Messi na Ronaldo wakiwakilisha Hispania ambayo iko kwenye eneo la kusini mwa Ulaya.

Wachezaji wengine nyota kama Zlatan Ibrahimovic, Gareth Bale, Neymar na Edinason Cavanni pia wanaweza kujumuishwa kwenye kikosi cha Ulaya Kusini ambacho kitakuwa na klabu za mataifa kutoka Ureno, Hispania na Ufaransa.

Wachezaji kama Wayne Rooney, Angel Dim Maria, Sergio Aguerro, Alexis Sanchez na Edin Hazard pamoja na wachezaji nyota wa Bayern Munich watawakilisha kikosi cha klabu za Ulaya Kaskazini.

Hata hivyo bado wazo hili halijawa rasmi na haijafahamika kama litafanyiwa kazi kikamilifu na kuweza kutimiza azma ya mashabiki ya kuona mkusanyiko wa wachezaji nyota wakiwa wanacheza kwenye timu moja.

millardayo.com ndio sehemu yako kuzipata story zote mtu wangu, unaweza kuwa karibu zaidi na mimi kwa kujiunga kwenye Facebook, Twitter na Instagram pia zitakufikia zote mtu wangu, jiunge hapa >>>twitter Insta Facebook

You Might Also Like

Samatta amerejea KRC Genk ya Ubelgiji

Manara na Wana-Yanga wakomaa kuwa kejeli Simba ‘Mlete Mzunguu’

Club ya Wolves ya England kuleta makocha wawili Tanzania

Inter Milan wawapa Yanga cha kusema, Shaffi Dauda atia neno, Manara apigilia msumari

Barbara awatuliza mashabiki wa Simba, wataka Mzungu aachwe wana mashabiki na mbinu za Kocha

TAGGED: Cristian Ronaldo, duniani, Lionel Messi
Millard Ayo April 14, 2015
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Umeona mastaa wa Club ya REAL MADRID wanavyojiachia? Cheki PICHAZ..
Next Article Jamaa alisinzia kwenye sehemu inayowekwa mizigo ndani ya ndege, kilichofuatia hapo ni ishu..
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Utacheka: Mwijaku apanda gari la Diamond ‘Rolls Royce’, Zuchu aangua kicheko, Baba Levo atia neno
Entertainment August 19, 2022
Picha: Diamond ameingia makubaliano ya kudhamini mashindano ya Ndondo Cup
Entertainment August 19, 2022
Kuelekea Sensa Agosti 23, Mbunge wa Jimbo la Ushtu anena hili kwa Wananchi wake
Top Stories August 19, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 19, 2022
Magazeti August 19, 2022

You Might also Like

Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 18, 2022

August 18, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 16, 2022

August 16, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 15, 2022

August 15, 2022
Magazeti

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 14, 2022

August 14, 2022
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?