Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Tanesco kuvuna Bilioni 5 ya mwezi kutoka GGM
Share
Notification Show More
Latest News
Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama
February 2, 2023
Habari kubwa Magazetini Kenya leo February 2, 2023
February 2, 2023
Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha
February 2, 2023
Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro
February 2, 2023
Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu
February 2, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Tanesco kuvuna Bilioni 5 ya mwezi kutoka GGM
Top Stories

Tanesco kuvuna Bilioni 5 ya mwezi kutoka GGM

February 22, 2022
Share
2 Min Read
.
SHARE

Kukamilika kwa mradi wa kupeleka umeme kwenye Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Geita Gold Mining (GGM) kutaliwezesha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupata kiasi cha shilingi bilioni 5 kwa mwezi zitakazotokana na mauzo ya umeme.

Hayo yamebanika Februari 21, 2022 wakati wa shughuli ya utiaji saini mkataba wa mauziano ya nishati ya umeme baina ya TANESCO na GGM.

Akiongea katika zoezi hilo Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Maharage Chande amesema kuanza kwa biashara hiyo kutaiwezesha TANESCO kuongeza mapato yatakayosaidia kuboresha huduma mbalimbali kwa wateja wao.

.

“Maana ya pili tutapunguza uzalishaji wa hewa chakafu ya dizeli, lakini pia kuongeza ufanisi wa kazi zao GGM kwa maana ya gharama za uzalishaji zitapungua” alisema Maharage.

Aliongeza kuwa, hatua hiyo kubwa na muhimu ya GGM kuunganishwa na umeme wa gridi ya Taifa imefikiwa baada ya miaka zaidi ya ishirini tangu kuanzishwa kwa kampuni ya GGM.

Kufanikiwa Kwa jambo hilo kumetokana  na jitihada mbalimbali zilizofanywa na TANESCO katika kuimarisha upatikanaji wa umeme ndani ya Mkoa wa Geita kwa kujenga kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mpomvu chenye uwezo wa megawati 90.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa GGM, Simon Shayo amesema GGM watajenga kituo cha kupokea na kupoza umeme kutoka kilovolti 33 hadi 11 ambazo zitatumika kwa matumizi ya mgodi.

“Kwetu sisi tunapunguza gharama za uzalishaji wa umeme tunao utumia kwa maana kwa kuacha kutumia mafuta lakini pia kutunza mazingira, Dunia sasa inatoka kwenye  matumizi ya mafuta ambayo yanazalisha hewa ya ukaa” amesema Shayo.

Kampuni ya GGM Kwa sasa inatumia senti 19 dola za kimarekani kuzalisha umeme kwa unit moja kwa kutumia mafuta, ambapo mradi huo ukikamilika na kuunganishwa na gridi watatumia senti 9  za kimarekani kwa unit moja kupata umeme.

Mradi huo wa kupeleka umeme GGM unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu,  ambapo utajumuisha njia ya kusafirisha umeme umbali wa kilometa 6 na kituo cha kupoza umeme cha GGM.

You Might Also Like

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama

Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha

Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro

Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu

liganga na Mchuchuma ngoma nzito, Waziri akubali hoja za Askofu Gwajima

Edwin TZA February 22, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Macvoice ametuletea hii collabo yake akiwa na Mbosso, itazame hapa
Next Article Jaji atupilia mbali mapingamizi kesi mgogoro wa ardhi Arusha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama
Top Stories February 2, 2023
Habari kubwa Magazetini Kenya leo February 2, 2023
Magazeti February 2, 2023
Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha
Top Stories February 2, 2023
Watu 60809 wapata Elimu ya Sheria Morogoro
Top Stories February 2, 2023

You Might also Like

Top Stories

Alhamisi ya TBT: Video 10 za kitambo kutokea Marekani hautozijutia kuzitazama

February 2, 2023
Top Stories

Utaipenda: Muonekano mpya wa Ilala, namna Bilioni 120 ilivyoibadilisha

February 2, 2023
Top Stories

Video: Mama amwaga machozi mbele ya Mwenyekiti wa umoja wa UVCCM, Rais Samia amtumia ujumbe huu

February 2, 2023
Top Stories

liganga na Mchuchuma ngoma nzito, Waziri akubali hoja za Askofu Gwajima

February 2, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?